MABAO ya Kieran Tierney dakika ya 23, Bukayo Saka dakika ya 28 na Alexandre Lacazette mawili dakika ya 60 na 64 jana yaliipa Arsenal ushindi wa 4-0 dhidi ya wenyeji, West Bromwich Albion kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa The Hawthorns.
Kwa ushindi huo The Gunners inafikisha pointi 23 na kusogea nafasi ya 11, ikizidiwa pointi tatu na wapinzani wao wa London, West Ham United baada ya wote kucheza mechi 17 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment