TIMU ya Arsenal jana imelazimishwa sare ya 0-0 na Crystal Palace katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Emirates, wimbi lao la ushindi wa mechi tatu mfululizo likikatishwa na kikosi cha Roy Hodgson.
Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta anapaswa kumshukuru mno kipa Bernd Leno kwa kuokoa mchomo mkali wa Christian Benteke. Arsenal inabaki nafasi ya 11 na pointi zake 24 za mechi 18, wakati Crystal Palace inabaki nafasi ya 13 na pointi zake 23 za mechi 18 pia PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment