BAO pekee la Mason Mount dakika ya 78 jana limeipa ushindi wa 1-0 Chelsea dhidi ya wenyeji, Fulham waliomaliza pungufu baada ya beki Mmarekani, Antonee Robinson kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 44 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa Craven Cottage.
The Blues wanafikisha pointi 29 baada ya kucheza mechi 18 na kupanda kwa nafasi tatu hadi ya saba, wakiizidi Arsenal pointi tano ambayo inashika nafasi ya 11 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment