MABAO ya Wilfred Ndidi dakika ya sita na James Maddison dakika ya 41 jana yaliipa Leicester City ushindi wa 2-0 dhidi ya Chelsea kwenye mchezo wa Ligi Kuu ya England Uwanja wa King Power.
Kwa ushindi huo, Leicester City inafikisha pointi 38 baada ya kucheza mechi 19 na kuendelea kuongoza Ligi Kuu ya England kwa pointi moja zaidi ya Manchester United iliyocheza mechi 18 ambayo leo inaifuata Fulham PICHA ZAIDI GONGA HAPA
0 comments:
Post a Comment