• HABARI MPYA

    Friday, September 15, 2017

    ZESCO UNITED WAIKOMALIA SUPERSPORT 0-0

    TIMU ya SuperSport United leo imelazimishwa sare ya 0-0 na Zesco United katikaa mchezo wa kwanza wa Robo Fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika Uwanja wa Lucas Moripe mjini Pretoria.
    Zesco ya Zambia sasa itakuwa mwenyeji wa SuperSport ya Afrika Kusini katika mchezo wa marudiano Uwanja wa Levy Mwanawasa Stadium mjini Ndola Jumamosi ijayo.
    Michuano hiyo itaendelea kesho kwa mechi tatu kupigwa; Uwanja wa Al-Ubayyid mjini Al Obayed, wenyeji Al Hilal Al Ubayyid wataikaribisha TP Mazembe ya DRC kuanzia Saa 2:00 usiku, Uwanja wa Moulay Hassan mjini Rabat, wenyeji FUS Rabat wataikaribisha CS Sfaxien ya Tunisia kuanzia Saa 4:30 usiku wakati Uwanja wa Julai 5, MC Alger wataikaribisha Club Africain ya Tunisia pia.
    Kikosi cha SuperSport kilikuwa: Williams, Kekana, Daniels, Gould, Modiba, Letsholonyane, Furman, Phala, Mnyamane/Wome dk69, Grobler/Mbule dk77 na Brockie
    Zesco: Banda, Silwimba, Owino, Musekwa, Kapumbu, Chaila, Mtonga, Daka/Kambole dk81, Ching'andu, Kalengo/Kasiyre dk88 na Were.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ZESCO UNITED WAIKOMALIA SUPERSPORT 0-0 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top