Kwa ushindi huo, Simba was SC inafikisha pointi 21 katika mchezo wa 10 na kusogea nafasi ya pili, ikizidiwa pointi mbili na vinara, Azam FC ambao pia wamecheza mechi moja zaidi.
Mabingwa watetezi, Yanga wanashukia nafasi ya tatu sasa na pointi zao 20 za mechi nane, ingawa kesho unaweza kurejea kileleni kama itashinda dhidi ya Kagera Sugar Jijini Mwanza.
Ihefu yenyewe baada ya kichapo cha leo hali inazidi kuwa mbaya, ikiendelea kushika mkia kwa pointi zake tano za mechi 10 sasa.
0 comments:
Post a Comment