• HABARI MPYA

    Sunday, November 13, 2022

    SIMBA QUEENS NAFASI YA NNE IMETOSHA LIGI YA MABINGWA


    TIMU ya Simba Queens jana ilimaliza nafasi ya nne kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Wanawake Afrika baada ya kuchapwa 1-0 na Bayelsa Queens ya Nigeria bao pelee la mshambuliaji Juliet Chinonso Uwanja wa Prince Moulay El Hassan Jijini Rabat nchini Morocco.
    Kwa kushika nafasi ya tatu, Simba Queens itazawadiwa kitita cha dola za Kimarekani 200,000 sawa na Bayelsa Queens kama wana Nusu Fainali, wakati bingwa atapata dola 400,000 na mshindi wa pili dola 250,000.
    Timu mbili zilizomaliza nafasi ya tatu katika makundi dola 150,000 kila moja na nyingine mbili zilizoshika mkia dola 100,000 kila moja.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA QUEENS NAFASI YA NNE IMETOSHA LIGI YA MABINGWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top