• HABARI MPYA

    Sunday, November 13, 2022

    MBEYA CITY YALAZIMISHWA SARE 2-2 NA COASTAL UNION SOKOINE


    WENYEJI, Mbeya City wamelazimishwa sare ya kufungana mabao 2-2 na Coastal Union katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Sokoine Jijini Mbeya.
    Mabao ya Mbeya City yamefungwa na Sixtus Sabilo yote dakika ya 39 na lingine kwa penalti dakika ya 80, wakati ya Coastal Union yamefungwa na Greyson Gwalala dakika ya 24 na Hamad Majimengi dakika ya 68.
    Kwa matokeo hayo, Mbeya City inafikisha pointi 16 katika mchezo wa 10 na kusogea nafasi ya tano, wakati Coastal Union nayo sasa ina pointi 12 za mechi tisa nafasi ya 11.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MBEYA CITY YALAZIMISHWA SARE 2-2 NA COASTAL UNION SOKOINE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top