• HABARI MPYA

    Monday, October 10, 2022

    SERENGETI BOYS YATINGA NUSU FAINALI CECAFA U17


    TIMU ya taifa ya Tanzania imefanikiwa kutinga Nusu Fainali ya michuano ya CECAFA U17 baada ya ushindi wa 2-1 dhidi ya Somalia jana Uwanja wa Abebe Bikila Jijini Addis Ababa nchini Ethiopia.
    Mabao ya Serengeti Boys katika mchezo huo wa mwisho wa Kundi A yote yamefungwa na Sylvester Otto dakika ya 75 na 80 na kwa matokeo hayo wanamaliza na pointi sita kufuatia awali kuwafunga wenyeji, Ethiopia 3-2.
    Sasa Serengeti Boys itamenyana na Sudan Kusini katika Nusu Fainali Jumatano, wakati Uganda ambao ndio mabingwa watetezi watacheza na Somalia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SERENGETI BOYS YATINGA NUSU FAINALI CECAFA U17 Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top