TIMU Taifa ya Tanzania chini ya Umri wa Miaka 20, Ngorongoro Heroes jana ilianza vibaya michuano ya kuwania kufuzu AFCON U20 baada ya kuchapwa 2-0 na Uganda katika mchezo wa Kundi B Uwanja wa Al Hilal nchini Sudan.
Ngorongoro Heroes itateremka tena dimbani Novemba 2 kumenyana na Ethiopia kukamilisha mechi zake za Kundi B ikihitaji lazima ushindi mzuri ili iende Nusu Fainali.
Ikumbukwe Kundi A linaundwa na Djibouti, Burundi, Sudan Kusini na Sudan.
0 comments:
Post a Comment