TIMU ya taifa ya wasichana U17 imeanza vibaya Fainali za Kombe la Dunia baada ya kuchapwa mabao 4-0 na Japan katika mchezo wa Kundi D leo Uwanja wa Jawaharlal Nehru (Fatorda Stadium) huko Margao, Goa nchini India.
Serengeti Girls itateremka tena dimba Jumamosi kumenyana na Ufaransa katika mechi wake wa pili wa Kundi D – kabla ya kukamilisha mechi zake za Kundi hilo kwa kumenyana na Canada Jumanne ijayo.
0 comments:
Post a Comment