• HABARI MPYA

    Monday, October 17, 2022

    REAL MADRID YAIFUMUA BARCA 3-1 BERNABEU


    WENYEJI, Real Madrid wameibuka na ushindi wa 3-1 dhidi ya Barcelona katika El Clasico ya 250 jana Uwanja wa Santiago Bernabeu Jijini Madrid na kupanda kileleni mwa La Liga.
    Mabao ya Real Madrid yamefungwa na Karim Benzema dakika ya 12, Fede Valverde dakika ya 35 na Rodrygo kwa penalti dakika ya 90 na ushei, wakati la Barcelona lilifungwa na Ferran Torres dakika ya 83. 
    Kwa matokeo hayo, Real Madrid wanafikisha pointi 25 na sasa wanaongoza La Liga kwa pointi tatu zaidi ya mahasimu wao hao, Barcelona kufuatia wote kucheza mechi tisa. 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REAL MADRID YAIFUMUA BARCA 3-1 BERNABEU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top