• HABARI MPYA

    Tuesday, October 25, 2022

    MTIBWA SUGAR YAICHAPA DODOMA JIJI 1-0 LITI


    BAO pekee la Charles Ilamfya dakika ya 60 limetosha kuipa Mtibwa Sugar ushindi wa 1-0 dhidi ya Dodoma Jiji FC Uwanja wa LITI mjini Singida.
    Kwa ushindi huo, Mtibwa Sugar inafikisha pointi 15 katika mchezo wa tisa na kupanda kileleni mwa Ligi Kuu ikizizidi pointi moja moja Simba na Yanga ambazo hata hivyo zimecheza mechi sita kila moja.
    Kwa upande wao, Dodoma Jiji FC wanabaki na pointi zao tano za mechi nane wakiendelea kushika mkia.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MTIBWA SUGAR YAICHAPA DODOMA JIJI 1-0 LITI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top