BAO la kichwa cha kupaa cha Marcus Rashford dakika ya 37 limeipa Manchester United ushindi wa 1-0 dhidi ya West Ham katika mchezo wa Ligi Kuu ya England leo Uwanja wa Old Trafford Jijini Manchester.
Kwa ushindi huo, Man United ya kocha Mholanzi, Erik ten Hag inafikisha pointi 23 katika mchezo wa 12 na kusogea nafasi ya tano ikiizidi pointi mbili Chelsea, wakati West Ham inabaki na pointi zake 14 za mechi 13 nafasi ya 13.
0 comments:
Post a Comment