BAO la Charles Ilamfya dakika ya 63 limetosha kuipa Mtibwa Sugar ushindi wa 1-0 dhidi ya Singida Big Stars katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara leo Uwanja wa Azam Complex, Chamazi nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Kwa ushindi huo, Mtibwa Sugar inafikisha pointi 12 katika mchezo wa nane na kusogea nafasi ya tatu, wakati Singida Big Stars inabaki na pointi zake nane za mechi sita nafasi ya 10.
0 comments:
Post a Comment