TANZANIA imeanza vyema michuano ya CECAFA U17 baada ya ushindi wa 3-2 dhidi ya wenyeji, Ethiopia leo katika mchezo wa Kundi A Uwanja wa Abebe Bikila Jijini Addis Ababa.
Mabao ya Tanzania, Serengeti Boys yamefungwa na Sylvester Otto mawili dakika ya tatu na 16 na Idrisa Makwepa dakika ya 86 na sasa vijana hao watateremka tena dimbani Jumapili kukamilisha mechi zao za Kundi hilo kwa kumenyana na Somalia.
Ikumbukwe Kundi B linaundwa na Uganda, Burundi na Sudan Kusini na bingwa wa michuano hiyo atashiriki AFCON U17.
0 comments:
Post a Comment