WENYEJI, Chelsea wameitandika AC Milan mabao 3-0 katika mchezo wa Kundi E Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku wa jana Uwanja wa Stamford Bridge Jijini London.
Mabao ya Chelsea yamefungwa na Wesley Fofana dakika ya 24, Pierre-Emerick Aubameyang dakika ya 56 na Reece James dakika ya 62.
Kwa matokeo hayo, Chelsea inafikisha pointi nne na kusogea nafasi ya pili, nyuma ya Salzburg yenye pointi tano, wakati AC Milan inayobaki na pointi zake nne inashukia nafasi ya tatu ikizidiwa wastani wa mabao na The Blues.
0 comments:
Post a Comment