• HABARI MPYA

    Thursday, July 01, 2021

    MESSI AMALIZA MKATABA BARCELONA NA HAKUNA ANAYEMTAKA

    MKATABA  wa Lionel Messi umemalizika jana Barcelona na hadi sasa hakuna taarifa zozote juu ya nyota huyo, ingawa matarajio ni atabaki.
    Messi mwenye umri wa miaka 34 ambaye kwa sasa yupo timu yake ya taifa, Argentina kwenye michuano ya Copa America, ilielezwa kwamba alishafikia makubaliano ya kuongeza mkataba kwa miaka miwili zaidi.
    Lakini mustakabali wa Messi haueleweki tangu aombe kuondoka mwenyewe mwishoni mwa msimu wa 2019-20, ingawa alibaki na akasema ataamua hatima yake mwishoni mwa msimu huo.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MESSI AMALIZA MKATABA BARCELONA NA HAKUNA ANAYEMTAKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top