• HABARI MPYA

    Sunday, July 18, 2021

    BUCKS YAIBWAGA SUNS 123-119 MECHI YA TANO FAINALI NBA

    TIMU ya Milwaukee Bucks imeibuka na ushindi wa 123-119 dhidi ya Phoenix Suns katika mechi ya tano ya Fainali za Ligi ya Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) Alfajiri ya leo ukumbi wa  Footprint Center, Phoenix, Arizona. 
    Pongezi kwao, Giannis Antetokounmpo aliyefunga pointi 32, rebounds tisa na assists sita, Khris Middleton pointi 29 na Jrue Holiday pointi 27 na assists 13.
    Sasa Milwaukee Bucks inaongoza kwa ushindi wa mechi 3-2 baada ya mwanzo mzuri wa Phoenix Suns kuongoza 2-0 baada ya mechi mbili za mwanzi na wakishinda mechi ya sita Alfajiri ya Jumatano nyumbani, watatwaa taji la kwanza la NBA 1971.

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BUCKS YAIBWAGA SUNS 123-119 MECHI YA TANO FAINALI NBA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top