• HABARI MPYA

    Monday, July 19, 2021

    BOCCO AWA MFUNGAJI BORA WA KWANZA MZAWA LIGI KUU BAADA YA WAGENI KUTAWALA MIAKA MITATU MFULULIZO

    MSHAMBULIAJI na Nahodha wa Simba amibuka mfungaji bora wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2020-2021 akiiwezesha klabu kutwaa taji la nne mfululizo.
    Bocco amemaliza msimu na mabao 16, akifuatiwa na wageni, Mkongo Chris Kope Mugalu 15 na Mzimbabwe Prince Dube Mpumelelo 14.
    Bocco anakuwa mfungaji bora wa kwanza mzawa tangu Simon Msuva alipochukua kwa pamoja na Abrhaman Mussa mwaka 2017.
    Baada ya hapo ni wageni waliotawala, Mganda Emmanuel Okwi 2018 na Mnyarwanda Meddie Kagere mara mbili mfululizo 2019 na 2020.


    ORODHA YA WAFUNGAJI BORA TANGU 2010:
    2010: MUSSA MGOSI (SIMBA SC) MABAO 18
    2011: MRISHO NGASSA (AZAM) MABAO 18
    2012: JOHN BOCCO (AZAM) MABAO 19 
    2013: AMISI TAMBWE  (SIMBA SC) MABAO 19
    2014: KIPRE TCHETCHE (AZAM FC) MABAO 17 
    2015: SIMON MSUVA (YANGA SC) MABAO 17
    2016: AMISI TAMBWE (YANGA SC) MABAO 21
    2017: SIMON MSUVA (YANGA SC) NA ABRAHMAN MUSSA (RUVU SHOOTING )MABAO 14
    2018: EMANUEL OKWI (SIMBA SC) MABAO 20
    2019: MEDDIE KAGERE MABAO 23
    2020: MEDDIE KAGERE (SIMBA SC) MABAO 22
    2021: JOHN BOCCO (SIMBA SC) MABAO 16
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BOCCO AWA MFUNGAJI BORA WA KWANZA MZAWA LIGI KUU BAADA YA WAGENI KUTAWALA MIAKA MITATU MFULULIZO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top