• HABARI MPYA

    Thursday, July 22, 2021

    YANGA SC YASTAAJABISHWA NA TFF KUPANGA REFA ALIYECHEZESHA MECHI MBILI MFULULIZO ZILIZOPITA ZA SIMBA ZA ASFC MWAKA HUU


    KLABU ya Yanga imelitaka Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kutafakari juu ya kumtumia refa Ahmed Arajiga katika mchezo wa F
    ainali ya Kombe la Shirikisho hilo, maarufu kama Azam Sports Federation Cup (ASFC) Jumapili mjini Kigoma.
    Yanga SC imedai masikitiko yao yanatokana na ukweli kwamba TFF ilimpanga refa huyo huyo kuchezesha mechi za wapinzani wao, Simba za Robo Fainali na Nusu Fainali wakizitoa timu za Dodoma Jiji FC na Azam FC.


    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: YANGA SC YASTAAJABISHWA NA TFF KUPANGA REFA ALIYECHEZESHA MECHI MBILI MFULULIZO ZILIZOPITA ZA SIMBA ZA ASFC MWAKA HUU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top