• HABARI MPYA

    Tuesday, July 27, 2021

    TANZANIA YATINGA FAINALI MICHUANO YA CECAFA CHALLENGE U23 BAADA YA KUICHAPA U23 SUDAN KUSINI 1-0 ETHIOPIA

    TANZANIA imefanikiwa kwenda Fainali ya Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati kwa vijana chini ya umri wamiaka 23 (CECAFA Challenge U23) baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Sudan Kusini mchana wa leo Uwanja wa Bahir dar nchini Ethiopia.
    Pongezi kwa mfungaji wa bao hilo pekee, Kelvin Nashon Naftali dakika ya 64 na sasa Tanzania itamenyana na mshindi wa Nusu Fainali ya pili inayoendelea hivi sasa baina ya Burundi na Kenya.
    Mechi ya Fainali itafanyika Ijumaa baada ya kutafutwa mshindi wa tatu Ijumaa hapo hapo Bahir Dar.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TANZANIA YATINGA FAINALI MICHUANO YA CECAFA CHALLENGE U23 BAADA YA KUICHAPA U23 SUDAN KUSINI 1-0 ETHIOPIA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top