KOCHA Mdenmark, Kim Poulsen ametaja kikosi wachezaji 20 wa timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 23 kitakachoingia kambini Julai 19, mwaka huu kwa ajili mashindano ya CECAFA Challenge U23.
Katika kikosi hicho, Poulsen amemjumuisha kipa aliyesimamishwa Yanga SC kwa utovu wa nidhamu, Metacha Boniphace Mata pamoja na wachezaji watatu waliozidi umri kwa mujibu wa kanuni za mashindano; Sospeter Israel wa Azam FC, Reliant Lusajo wa Namungo FC na Yussuph Mhilu wa Kagera Sugar.
0 comments:
Post a Comment