• HABARI MPYA

    Friday, January 08, 2021

    MIRAJ ATHUMANI ‘MADENGE’ APIGA MBILI SIMBA SC YAICHAPA CHIPUKIZI 3-1 KOMBE LA MAPINDUZI

    Na Mwandishi Wetu, ZANZIBAR
    SIMBA SC imeanza vyema michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya ushindi wa 3-1 dhidi ya wenyeji, Chipukizi FC ya Pemba kwenye mchezo wa Kundi B jioni ya leo Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
    Pongezi kwake Miraj Athumani ‘Madenge’ aliyefunga mabao mawili dakika ya 53 na 83 baada ya mshambuliaji mwingine, Mnyarwanda Meddie Kagere kufunga la kwanza dakika ya 45 kufuatia Chipukizi kutangulia kwa bao la Fakhi Mwalimu Sharrif dakika 36.
    Mchezo wa Kundi A baina ya vigogo, Yanga SC ya Dar es Salaam na Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi inafuatia hivi sasa hapo hapo Uwanja wa Amaan.


    MAKUNDI
    Kundi B; Simba SC, Mtibwa Sugar, Chipukizi FC.
    Kundi A; Yanga SC, Namungo FC, Jamhuri FC
    Kundi C; Azam FC, Malindi FC, Mlandege FC
    MATOKEO NA RATIBA 
    Januari 5, 2021
    Yanga SC 0-0 Jamhuri
    Mtibwa Sugar 1-0 Chipukizi
    Januari 6, 2021
    Malindi FC 0-0 Mlandege
    Januari 7, 2021
    Azam FC 1-1 Mlandege FC
    Januari 8, 2021
    Simba SC 3-1 Chipukizi
    Yanga SC v Namungo FC
    Januari 9, 2021
    Azam FC v Malindi FC
    Januari 10, 2021
    Jamhuri FC v Namungo FC
    Simba SC v Mtibwa sugar
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MIRAJ ATHUMANI ‘MADENGE’ APIGA MBILI SIMBA SC YAICHAPA CHIPUKIZI 3-1 KOMBE LA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top