Mkongwe Fabio Quagliarella akishangilia baada ya kuifungia mabao mawili Italia dakika za 35 na 45 na ushei yote kwa penalti katika ushindi wa 6-0 dhidi ya Liechtenstein kwenye mchezo wa Kundi J kufuzu Euro 2020 usiku wa jana Uwanja wa Ennio Tardini mjini Parma. Mabao mengine ya Italia yalifungwa na Stefano Sensi dakika ya 17, Marco Verratti dakika ya 32, Moise Kean dakika ya 69 na Leonardo Pavoletti dakika ya 76 na kwa ushindi huo The Azzurri inafikisha pointi sita kufuatia kushinda mechi zake zote mbili za mwanzo ikifuatiwa na Ugiriki yenye pointi nne. Mechi nyingine za kundi hilo jana Bosnia-Herzegovina ililazimishwa sare ya 2-2 Ugiriki mjini Zenica na Finland ikawachapa wenyeji, Armenia 2-0 PICHA ZAIDI GONGA HAPA
West Ham 2-2 Brentford (pens 5-3): Hammers earn FA Cup quarter-final spot
after nerve-wracking clash - after Dango Ouattara hits EMBARRASSING
spot-kick
-
LUKE POWER AT THE LONDON STADIUM: West Ham booked their place in the
quarter-finals of the FA Cup for the first time in a decade - and had a
woeful Panenka...
47 minutes ago



.png)
0 comments:
Post a Comment