• HABARI MPYA

    Monday, November 26, 2018

    REFAWA KIKE WA TANZANIA, JONESYA RUKYAA KUCHEZESHA NUSU FAINALI YA AFCON YA WANAWAKE KESHO GHANA

    Na Mwandishi Wetu, DAR ES SALAAM
    REFA wa Tanzania Jonesya Rukyaa atachezesha mchezo wa nusu Fainali ya Afcon ya Wanawake inayoendelea nchini Ghana.
    Rukyaa atakuwa Mwamuzi wa katikati kwenye mchezo wa South Africa dhidi ya Mali utakaochezwa kesho Novemba 27,2018 saa 12:30 jioni Cape Coast Sports Stadium.
    Katika mchezo huo Rukyaa atasaidiwa na Mwamuzi msaidizi namba 1 Mona Mahmoud Atallah wa Misri,Mwamuzi msaidizi namba 2 Adia Isseu Cisse wa Senegal na Mwamuzi wa akiba Suavis Iratunga wa Burundi 
    Rukyaa mwenye beji ya FIFA ndio Mwamuzi pekee kutoka Tanzania aliyeteuliwa kuchezesha Fainali hizo za Afrika kwa Wanawake.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: REFAWA KIKE WA TANZANIA, JONESYA RUKYAA KUCHEZESHA NUSU FAINALI YA AFCON YA WANAWAKE KESHO GHANA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top