![]() |
| Free State wakisherehekea ushindi wao wa SAB U21 ya Afrika Kusini |
Michuano hiyo ya saba ya U21 inayoandaliwa na Chama cha Soka Afrika Kusini (SAFA) chini ya udhamini wa Kampuni ya Bia Afrika Kusini (SAB), ilifanyika Uwanja wa Giant mjini Soshanguve.
Na Free State ambayo imemsajili Mrisho Ngassa wa Tanzania Mei mwaka huu kwa ajili ya kikosi cha kwanza, imeweka historia kwa kuwa timu ya kwanza kutetea taji hilo. Haukuwa ushindi mwepesi kwa Free State kwani walilazimika kuifunga timu ambayo imetoa mfungaji bora wa mashinfdano na mchezaji borsa, Siphamandla Dhlamini.
Wasaka vipaji kadhaa walimiminika kwenye michuano hiyo ambayo imekuwa ikizalisha nyota kibao wa taifa hilo kusaka vipaji vya kupandisha Ligi Kuu.
SAFARI YA FREE STATE HADI UBINGWA SAB U21 2015
Mpumalanga
1. Free State 2 – 1 Mpumalanga
2. Mpumalanga 2 – 1 Western Cape
3. Mpumalanga 4 - 1 Gauteng
4. Mpumalanga 4 – 1 Northern Cape
Free State
1. Free State 2 – 1 Mpumalanga
2. Gauteng 2 – 3 Free State
3. Free State 2 – 3 Northern Cape
4. Free State 3 – 0 Western Cape
Nusu Fainali
Mpumalanga 4 – 2 University Sport SA
Limpopo 0 – 2 Free States
Fainali:
Mpumalanga (1) 1 – 1 (3) Free State
WASHINDI WA TUZO ZA SAB U21
Mwamuzi Bora Msaidizi: Bafana Magagula
Refa Bora: Khotso Johanne
Kocha Bora: Litheko Marago
Mfungaji Bora: Siphamandla Dhlamini
Kipa Bora: Kwanele Bidi
Mchezaji Bora: Siphamandla Dhlamini



.png)
0 comments:
Post a Comment