BEKI Anton Ferdinand amesaini mkataba wa miaka miwili na Reading baada ya mwaka mmoja wa kutemwa na Queens Park Rangers.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 alikuwa akiichezea Antalyaspor lakini ameamua kuondoka Uturuki na kurudi nyumbani. Ilifikiriwa kwamba mdogo huyo wa Rio, aliyewahi kuchezea West Ham alikuwa tayari kusaini Mkataba na Polisi United ya Thailand, lakini akaamua kurejea England.
"Nimekuwa mbali na soka ya England kwa mwaka na nimekuwa na wakati fulani mgumu,"amesema Ferdinand. "Uturuki ni sehemu nzuri kwenda na kucheza soka, lakini mambo fulani nje ya Uwanja hayakunipa fursa ya kucheza soka yangu haswa,".



.png)
0 comments:
Post a Comment