KOCHA wa Uholanzi, Louis van Gaal amesema kwamba wachezaji wake wawili waligoma kupiga penalti ya kwanza jana wakitolewa na Argentina Katika Nusu Fainali Kombe la Dunia.
Uholanzi ilishindwa kurudia ilichokifanya Robo Fainali dhidi ya Costa Rica waliposhinda kwa penalti, baada ya beki wa Aston Villa, Ron Vlaar kukosa penalti ya kwanza na Wesley Sneijder pia akapoteza.
Argentina ilifunga penalti zote nne kujihakikishia kutinga Fainali ambako itamenyana na Ujerumani Uwanja wa Maracana Jumapili.
Baada ya mechi, Van Gaal - ambaye anakwenda kuanza kazi Manchester United wiki ijayo- alisema kwamba wachezaji wake wawili waligoma kupiga penalti ya kwanza.
"Unahitaji kufunga ya kwanza na niliwaomba wachezaji wawili kupiga mpira wa kwanza, nikamalizia na Vlaar. Nafikiri alikuwa mchezaji bora uwanjani, hivyo alikuwa anajiamini. Ikaonekana si rahisi kufunga katika matuta,"amesema.
Mkali wa matuta: Kipa wa Argentina, Sergio Romero akiokoa penalti ya kiungo Wesley Sneijder
0 comments:
Post a Comment