• HABARI MPYA

    Thursday, December 05, 2013

    UGANDA WAICHAPA SUDAN 1-0 NA KUJIHAKIKISHIA KUCHEZA NA BARA ROBO FAINALI, RWANDA NA KENYA, BURUNDI NZA ZAMBIA…

    Dan Sserunkuma wa Uganda akimtoka beki wa Sudan, Malik Mohamed katika mchezo wa Kundi C leo Uwanja wa Nyayo. Uganda ilishinda 1-0.
    Na Mahmoud Zubeiry, Nairobi
    BAO pekee la kiungo Khalid Aucho dakika ya 47, limeipa Uganda ushindi wa 1-0 Uganda dhidi ya Sudan katika mchezo wa mwisho wa Kundi C, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Uwanja wa Nyayo, Nairobi, Kenya jioni hii.

    ROBO FAINALI ZA CHALLENGE…

    Desemba 7, 2013;
    Uganda VS Tanzania
    Kenya   VS Rwanda
    Desemba 8, 2013
    Zambia   VS  Burundi
    Ethiopia  VS  Sudan
    Robo Fainali zitachezwa Uwanja wa Manispaa, Mombasa, Kenya Jumamosi na Jumapili
    Mshambuliaji wa zamani wa Simba SC, Emmanuel Okwi alicheza tangu mwanzo, lakini nyota wa Yanga SC, Hamisi Kiiza aliingia kipindi cha pili, wakati Dani Sserunkuma wa Gor Mahia alicheza kipindi cha kwanza pekee.
    Kocha wa zamani wa Yanga, Milutin Sredojevic ‘Micho’ alikuwa mwenye furaha baada ya mechi kwa sababu anakutana na Tanzania, ambayo aliifunga katika mechi za kufuzu za CHAN nyumbani na ugenini.
    Baada ya matokeo ya leo, Uganda imeongoza Kundi C kwa pointi zake tisa na Sudan imekuwa ya pili kwa pointi zake sita. Uganda itacheza na Tanzania Bara katika Robo Fanali, wakati Kenya itacheza na Rwanda, Zambia na Burundi na Ethiopia na  Sudan.
    Mechi zote za Robo Fainali zitachezwa Uwanja wa Manispaa mjini Mombasa Jumamosi na Jumapili, wakati Nusu Fainali zitarudi Nyayo, ingawa iwapo uwekaji nyasi bandia katika Uwanja wa Moi, Kisumu utawahi kukamilika basi Nne Bora zitachezwa na huko, wakati fainali ni Nairobi.
    Beki wa Uganda, Mpuga Martin akiruka juu kupiga mpira kichwa dhidi ya mshambuliaji wa Sudan, Salah Ibrahim
    Dani Sserunkuma akimtoka Malik Mohamed
    Emmanuel Okwi akimfunga tela beki wa Sudan
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: UGANDA WAICHAPA SUDAN 1-0 NA KUJIHAKIKISHIA KUCHEZA NA BARA ROBO FAINALI, RWANDA NA KENYA, BURUNDI NZA ZAMBIA… Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top