• HABARI MPYA

        Wednesday, December 18, 2013

        STRAIKA MPYA AZAM AONYESHA NI MOTO WA KUOTEA MBALI...MAANDALIZI YA KWENDA KUBEBA TENA MWALI WA MAPINDUZI YASHIKA KASI CHAMAZI

        Nahodha wa Azam FC, John Bocco 'Adebayor' akifanya mazoezi na wenzake leo asubuhi Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Azam inajiandaa kwenda kutetea Kombe la Mapinduzi, michuano inayoanza Januari 1, mwakani visiwani Zanzibar.
        Mshambuliaji tegemeo kutoka Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche akinywa maji ya Uhai baada ya mazoezi 
        Mshambuliaji mpya kutoka klabu ya Stella Abidjan ya Ivory Coast, Ismael Muamad Kone (katikati) akikokota mpira mazoezini leo. Kone ameonyesha ni mchezaji mzuri na wapenzi wa Azam watarajie kuona vitu vyake kuanzia Januari katika Kombe la Mapinduzi.
        Kone akinyoosha viungo
        Kiungo Jabir Aziz Stima akinyoosha viungo

        Kocha wa akademi, Vivik Nagul ndiye aliongoza mazoezi leo akishirikiana na kocha Msaidizi, Kali Ongala wakati kocha Mkuu, Joseph Marius Omog raia wa Cameroon atawasili Ijumaa
        Gaudence Mwaikimba akikokota mpira

        Mganda Brian Umony bado yupo Chamazi

        Kipa Mwadini Ally kushoto akidaka na kulia ni kocha wa makipa Iddi Abubakar Mwinchumu

        Beki tegemeo, Aggrey Morris akichezea mpira

        Kulia beki David Mwantika

        Kone ni hatari bosi; Meneja wa Azam akizungumza na simu wakati mazoezi yakiendelea

        Wachezaji wa kikosi cha kwanza walichanganyika na wachezaji wa akademi

        • Blogger Comments
        • Facebook Comments

        0 comments:

        Item Reviewed: STRAIKA MPYA AZAM AONYESHA NI MOTO WA KUOTEA MBALI...MAANDALIZI YA KWENDA KUBEBA TENA MWALI WA MAPINDUZI YASHIKA KASI CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry