• HABARI MPYA

    Tuesday, December 17, 2013

    SUAREZ ABEBA TUZO YA MWANASOKA BORA WA MWAKA

    MSHAMBULIAJI Luis Suarez ametajwa mchezaji bora wa mwaka wa tuzo ya Shirikisho la Mashabiki wa Soka jana usiku.
    Kiasi kisichozidi miezi sita baada Arsenal kutaka kumnunua kwa Pauni 40,000,001 nyota huyo wa Uruguay, Suarez aliinua tuzo hiyo Emirates.
    Lakini ilikuwa ni tuzo binafsi kwa mshambuliaji huyo wa anayemtoa udenda kocha Arsene Wenger, akiwapiku Leighton Baines, Christian Benteke, Juan Mata, Robin van Persie na Pablo Zabaleta kushinda tuzo hiyo iliyohusisha wapiga kura zaidi ya 500,000.
    Mshindi: Mchezaji Bora wa Mwaka, Luis Suarez akisherehekea tuzo yake ya Shirikisho ya Mashabiki wa Soka, akiwa na mkewe Sofia
    Mshambuliaji huyo wa Liverpool, aliyehudhuria shughuli hiyo Emirates, alisema: "Nafikiri ni haki kusema mwaka uliopita ulikuwa mzuri kwangu. 
    "Tuzo hii si yangu peke yangu, ni pamoja na wachezaji wenzangu, uongozi na benchi la Ufundi na yeyote anayehusiana na Liverpool,". 
    Eventful year: Suarez celebrates with his award at the Emirates Stadium
    Suarez akisherehekea na tuzo yake Uwanja wa Emirates
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SUAREZ ABEBA TUZO YA MWANASOKA BORA WA MWAKA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top