• HABARI MPYA

    Tuesday, December 31, 2013

    SIMBA SC WAKIWA SAFARINI ZANZIBAR KUFUATA 'NDOO' YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI

    Wachezaji wa Simba SC wakiwa eneo la bandari ndogo, Azam Marine, Dar es Salaam wakielekea kupanda boti asubuhi hii tayari kwa safari ya Zanzibar kwenda kushiriki Kombe la Mapinduzi, michuano inayoanza kesho visiwani humo.
    Kulia Said Ndemla 'Ozil', kushoto Nassor Masoud 'Chollo' na katikati Ramadhani Chombo 'Redondo'. Michuano ya mwaka huu itakwenda sambamba na sherehe za miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.
    Supa staa; Ramadhani Sngano 'Messi' hakuwa na sare ya timu kama wenzake
    Nahodha Chollo kushoto akimpa tiketi yake beki Mganda, Joseph Owino. Wengine kulia ni Daktari, Yaasin Gembe na Kocha Msaidizi, Suleiman Matola kushoto
    Chollo akimpa tiketi Amri Kiemba
    Kulia Redondo, katikati kocha wa makipa Iddi Pazi 'Father' na kushoto mshambuliaji Ali Badru
    Kipa Yaw Berko akiikagua tiketi yake baada ya kukabidhiwa na Nahodha Msaidizi, Haruna Shamte kushoto

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA SC WAKIWA SAFARINI ZANZIBAR KUFUATA 'NDOO' YA MIAKA 50 YA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top