• HABARI MPYA

    Friday, December 27, 2013

    AZAM YAENDA NA 33 MAPINDUZI, MCHEZAJI MPYA KUTOKA DRC ATUA CHAMAZI

    Na Mahmoud Zubeiry, Chamazi
    KIKOSI kizima cha Azam FC, kinatarajiwa kuondoka Dar es Salaam Januari 1, kuelekea visiwani Zanzibar kushiriki michuano ya Kombe la Mapinduzi.
    Meneja wa Azam FC, Jemadari Said Kazumari ameiambia BIN ZUBEIRY kwamba, Azam itaondoka na wachezaji 33 wakiwemo waliopandishwa kutoka akademi ya timu hiyo.
    Hata hivyo, katika kikosi hicho kiungo Mkenya, Humphrey Mieno anaweza kukosekana kutokana na kutowasili hadi sasa kujiunga na wenzake mazoezini.
    Jemadari alisema Mieno baada ya kupewa ruhusa ya awali hakurejea muda wake ulipomalizika na uongozi ulipowasiliana naye akasema ana matatizo ya kifamilia, hivyo akaongezewa muda ambao pia umeisha.

    Mabingwa watetezi: Azam ni mabingwa watetezi wa Kombe la Mapinduzi kwa miaka miwili mfululizo

    MSAFARA WA AZAM ZANZIBAR

    WACHEZAJI;
    AISHI SALLUM MANULA
    ABDALLAH SEIF KARIHE.
    AGGREY MORIS AMBROSI
    BRAISON RAFAEL NKULULA
    BRIAN UMOMY
    DAVID JOHN MWANTIKA
    ERASTO EDWARD NYONI
    FARID MUSSA SHAH
    GAUDENCE EXAVERY MWAIKIMBA
    GADIEL MICHAEL MBAGA
    HIMID MAO MKAMI
    IBRAHIM JOEL MWAIPOPO
    ISAMEL ADAM GAMBO
    JABIR AZIZ STIMA
    JOHN RAFAEL BOCCO
    JOSEPH LUBASHA KIMWAGA
    KELVIN FRIDAY IDD
    KIPRE HERMANN BRICE TCHETCHE
    KONE ISMAEL MOUHAMED
    KHAMIS MCHA KHAMIS
    LUCKSON JONATHAN KAKOLAKI
    BOLOU WIFRED MICHAEL KIPRE
    MALIKA PHILIPO NDEULE
    MUDATHIR YAHYA ABBASI
    MWADINI ALI MWADINI
    REYNA ELIMINIUS MGUNGILA
    SAID HUSSEIN MORADI
    SAMIH ALI NUHU
    SWALEHE ABDALLAH 
    WANDWI JACKSON WANDWI
    WAZIRI SALLUM OMAR
    SALLUM ABUBAKAR SALLUM
    HUMPHREY OCHIENG MIENO
    HAMADI JUMA HAMADI

    VIONGOZI.
    JOSEPH MARIUS OMOG
    KALIMANGONGA SAM DANIEL ONGALA
    IBRAHIM SHIKANDA CHIMWAGA
    IDD ABUBAKAR MWICHUMU
    VIVEK NAGUL
    MWANANDI JUMA MWANKEMWA
    VICENT JUMA MADEGE
    TWALIBU MBARAKA
    YUSUF DAVID NZAWILA
    SWALEHE JUMAPILI AWADHI
    JEMEDARI SAID KAZUMARI
    “Na bado tumekuwa tukimtumia ujumbe wa barua pepe na sms kumuuliza kulikoni amechelewa, lakini bado amekuwa hajibu, hivyo hatuelewi nini kimemkwamisha,”alisema.
    Aidha, Jemadari alisema wana mchezaji mpya mazoezini kutoka Don Bosco ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), Djunes Kayanda aliyewahi pia kuchezea Zanaco ya Zambia.
    Jemadari amesema mshambuliaji huyo wa pili ni kijana mdogo wa umri wa miaka 19 na ingawa kwa sasa hawezi kusajiliwa, lakini uongozi umeamua kumpa muda zaidi kuendelea kumtazama.
    Tayari Azam ina wachezaji watano wa kigeni, ambao ni kiungo Kipre Michael Balou na washambuliaji Kipre Herman Tchetche na Muamad Ismael Kone wote kutoka Ivory Coast pamoja na Mganda Brian Umony na Mkenya Mieno.
    Kone amesajiliwa msimu huu akichukua nafasi ya beki Mkenya, Joackins Atudo aliyetemwa baada ya kumaliza Mkataba wake.  
    Azam FC hivi sasa ipo chini ya kocha mpya, Joseph Marius Omog raia wa Cameroon ambaye mara ya mwisho alikuwa kocha wa klabu ya FC Leopard ya Kongo Brazzaville.
    Azam jana ilicheza mechi ya kwanza chini ya Omog na kushinda mabao 3-0 dhidi ya Ruvu Shooting ya Pwani katika mchezo wa kirafiki uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam jioni hii.
    Hadi mapumziko, tayari Azam FC, walio chini ya kocha mpya Mcameroon, Joseph Marius Omog walikuwa mbele kwa mabao 2-0.
    John Raphael Bocco alitangulia kuifungia Azam bao la kwanza dakika ya 10 kazi nzuri Mganda, Brian Umony ambaye anaonekana kurudi katika kasi yake ya mchezo baada ya kuandamwa na majeruhi msimu uliopita. 
    Bao la pili liliwekwa nyavuni kwa mkwaju wa penalti na mshambuliaji wa Ivory Coast, Kipre Herman Tchetche dakika ya 30, baada ya Ayoub Kitala kuurudisha kwa mkono mpira uliokuwa unaelekea nyavuni.
    Refa Israel Mujuni Nkongo alimpa kadi nyekundu beki wa Ruvu na kuifanya timu ya Charles Boniface Mkwasa ‘Master’ imalizie dakika 50 za pambano hilo ikiwa pungufu.
    Mchezo ulikuwa mzuri kipindi cha kwanza timu zote zikicheza soka ya kufundishwa na makocha waliosomea Ujerumani, Mkwasa wa Ruvu na Omog wa Azam FC.
    Kipindi cha pili timu zote zilifanya mabadiliko karibu ya vikosi vizima na aliyekuwa kivutio katika ngwe hiyo ni mshambuliaji mpya kutoka Ivory Coast Muamad Ismael Kone aliyeingia pia kwa upande wa Azam. 
    Kone alionyesha uwezo mkubwa sana wa kucheza soka na akafunga bao zuri la tatu dakika ya 57.
    Mchezaji mpya Djunes Kayanda kushoto mazoezini Chamazi
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: AZAM YAENDA NA 33 MAPINDUZI, MCHEZAJI MPYA KUTOKA DRC ATUA CHAMAZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top