• HABARI MPYA

    Wednesday, December 04, 2013

    ANKO NGASSA HAKUWAFUNGA SOMALIA, ATAWAWEZA BURUNDI LEO?

    Na Mahmoud Zubeiry, Nakuru
    MRISHO Khalfan Ngassa ‘Anko’ ni miongoni mwa wachezaji waliotarajiwa kung’ara katika michuano ya kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge mwaka huu nchini Kenya, lakini hadi sasa hafajatisha.
    Mshambuliaji huyo wa Yanga amecheza mechi mbili za makundi bila kufunga hata bao moja na katika mechi dhidi ya Somalia alitolewa dakika 79 kumpisha Farid Mussa.
    Ngassa akienda benchi amechaka matope dhidi ya Somalia, lakini hakufunga bao
     
    Tayari washambuliaji wawili wa TP Mazembe, Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu wamewasili Kenya kukiongezea nguvu kikosi cha Tanzania Bara, Kilimanjaro Stars na bila shaka kocha Kim Poulsen atawaanzisha wote leo.
    Na kama itakuwa hivyo, Ngassa atacheza pembeni katika mechi hiyo inayoanza saa 8:00 mchana wa leo, hivyo kuwa na jukumu la kuwatengenezea nafasi zaidi Samatta na Ulimwengu.
    Lakini kwa kuwa Samatta na Ulimwengu nao wakati mwingine husogea pembeni, Ngassa anaweza akawa na nafasi ya kufunga hata kwa kuingia moja kwa moja kutokea pembeni.
    Tayari mashabiki nchini Kenya wamekwishaanza kumpuuza Ngassa wakiamini makali yake yameanza kupata kutu, lakini ukweli wa yote utajulikana leo baada ya mechi na Burundi. Anko Ngassa aliyewakosa Somalia, atawapata Burundi leo? 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ANKO NGASSA HAKUWAFUNGA SOMALIA, ATAWAWEZA BURUNDI LEO? Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top