MTENDAJI Mkuu wa Simba SC, Imani Kajula akiwa makao makuu ya Shirikisho la Soka Afrika (CAF) Jijini Cairo nchini Misri leo kuiwakilisha klabu kwenye droo ya mech za Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika inayotarajiwa kupangwa leo kuanzia Saa 3:30 usiku.
Baada ya kumaliza nafasi ya pili kwenye Kundi C nyuma ya vinara, Raja Casablanca ya Morocco, Simba SC inatarajiwa kupangiwa ama mabingwa watetezi, Wydad Casablanca ya Morocco pia, Esperance ya Tunisia au Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini.
0 comments:
Post a Comment