• HABARI MPYA

    Saturday, October 01, 2022

    NAMUNGO FC NA KMC HAKUNA MBABE, 0-0 MAJALIWA


    WENYEJI, Namungo FC wamepanda kileleni mwa Ligi Kuu ya Tanzania Bara licha ya sare ya bila kufungana na KMC katika mchezo uliofanyika Uwanja wa Majaliwa, Ruangwa mkoani Lindi.
    Namungo FC inafikisha pointi 11 katika mchezo wa tano na kupanda juu ya msimamo, ikizizidi pointi moja moja zote Simba na Yanga ambazo hata hivyo zina mechi moja moja mkononi.
    Kwa upande wao, KMC wanafikisha pointi sita katika m hizo wa tano pia na kusogea nafasi ya tisa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: NAMUNGO FC NA KMC HAKUNA MBABE, 0-0 MAJALIWA Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top