• HABARI MPYA

    Friday, October 09, 2015

    TAIFA STARS WALIVYOFANYA MAZOEZI USIKU WA LEO BLANTYRE

    Wachezaji wa timu ya soka ya taifa ya Tanzania, 'Taifa Stars' wakifanya mazoezi mepesi usiku wa leo kwenye Uwanja wa klabu ya Michezo mjini Blantyre, Malawi kuelekea mchezo wa marudiano na wenyeji Jumapili hatua ya kwanza ya mchujo kuwania kupangwa kwenye makundi ya kuwania tiketi ya Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2018 nchini Urusi.
    Taifa Stars iliyowasili leo jioni mjini Blantyre baada ya safari kutwa nzima kutoka nzima kutoka Dar es Salaam kuanzia ndege hadi basi, ilishinda 2-0 katika mchezo wa kwanza nyumbani
    Pamoja na uchovu wa safari ya kutwa, lakini vijana walifanya mazoezi leo
    Jumapili Taifa Stars itahitaji hata sare ii kusonga mbele, ambako itakutana na Algeria katika hatua ya mwisho ya mchujo
    Wachezaji wote waliokuja na timu hapa wamefanya mazoezi leo
    Wachezaji wakiomba dua baada ya mazoezi yao usiku wa leo

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: TAIFA STARS WALIVYOFANYA MAZOEZI USIKU WA LEO BLANTYRE Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top