Kocha Mkuu wa Azam FC, Muingereza Stewart John Hall leo hatakaa katika benchi la timu yake ikimenyana na Yanga SC Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam katika mchezo wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara kwa sababu anatumikia adhabu baada ya kutolewa kwa kadi nyekundu katika mchezo uliopita dhidi ya Coastal Union Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es Salaam. Msaidizi wake namba moja, Mario Marinica ndiye ataongoza timu akisaidiwa na mzalendo Dennis Kitambi. |
0 comments:
Post a Comment