• HABARI MPYA

    Monday, April 06, 2015

    WENGER: SASA MAMBO YANAKUWA MAMBO ARSENAL

    KOCHA Arsene Wenger anashawishika kusema hatimaye mambo yanakuwa mambo Arsenal tena - na kila mmoja anaweza kuisikia harufu hiyo.
    The Gunners iliirarua 4-1 Liverpool Uwanja wa Emirates Jumamosi mchana, ambao ulikuwa ni ushindi wa saba mfululizo kwao katika Ligi Kuu ya England, ambao unawapandisha hadi nafasi ya pili.
    Wakati Manchester City inaweza kurudi nafasi ya pili iwapo itaifunga Crystal Palace leo, nyuma ya vinara Chelsea wanaaoongoza kwa pointi saba, hakuna shaka Wenger akiwa ana kikosi chake kamili ataendelea kupambana.
    Mesut Ozil is congratulated by his team-mates after his magnificent free-kick on the half hour mark put Arsenal fully in control of the game
    Mesut Ozil akipongezwa na wenzake baada ya kufunga Jumamosi dhidi ya Liverpool

    Hata hivyo, mafanikio haya yanakuja kwa Wenger baada ya kupitia msimu mgumu akitolewa kwenye michuano ya Ulaya na Monaco, na sasa nvuvu zote zipo kwenye kumaliza vizuri na kutetea Kombe la FA.
    "Tuko vizuri kwa sasa na tumeimarika kama timu. Kuna vitu vinatokea, ambavyo vinakuonyesha wewe kwamba wapo tayari kupambana kila mmoja,". Wenger amepanoa kuifunga Chelsea Uwanja wa Emirates Aprili 26 ili kupunguza pengo la pointi.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: WENGER: SASA MAMBO YANAKUWA MAMBO ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top