• HABARI MPYA

    Sunday, April 05, 2015

    LEWIS MPYA AENDELEZA VIPONDO ULINGONI, AMKALISHA MMAREKANI RAUNDI YA TATU

    MBABE mpya wa ndondi za uzito wa juu, Anthony Joshua amemsimamisha mpinzani wake, mzoefu Jason Gavern wa Marekani kwa Knockout (KO) raundi ya tatu katika pambano lisilo la ubingwa mjini Newcastle.
    Hata hivyo, bondia huyo wa Uingereza anayeitwa 'Lennox Lewis mpya' pamoja na kushinda pambano la 11 mfululizo tangu aanze ndondi za kupigana kifua wazi, hakufurahishwa na kiwango chake akisema hakuwa katika ubora wake jana.
    Gavern, akipigana pambano lake la 50, aliangushwa mara mbili katika raundi ya pili na akaangushwa tena katika raundi ya tatu pambano hilo likiishia hapo.
    Sasa, Joshua, ambaye alirejea ulingoni baada ya kukosekana kwa miezi mitano kutokana na majeruhi ya mgongo, atapambana na Kevin Johnson ukumbi wa O2, London Mei 30.
    Anthony Joshua lands a left hand on Jason Gavern on his way to another convincing victory
    Anthony Joshua akimchapa konde mpinzani wake, Jason Gavern 
    Anthony Joshua in action with Jason Gavern
    Anthony Joshua in action with Jason Gavern
    Joshua akimuadhibu mpinzani wake mjini Newcastle jana
    Joshua stands over the fallen Gavern as he boxed in front of the Newcastle crowd for the first time
    Joshua akiwa amesimama mbele ya Gavern aliyeanguka chini

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/boxing/article-3025978/Anthony-Joshua-stops-Jason-Gavern-warm-Kevin-Johnson-test.html#ixzz3WPElKVek 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: LEWIS MPYA AENDELEZA VIPONDO ULINGONI, AMKALISHA MMAREKANI RAUNDI YA TATU Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top