• HABARI MPYA

    Sunday, April 05, 2015

    BASI LA FENERBAHCE LASHAMBULIWA KWA MTUTU WA BUNDUKI

    BASI lililokuwa limebeba wachezaji wa timu ya Fenerbahce ya Uturuki na makocha wao, limeshambuliwa kwa risasi jana usiku.
    Gavana wa Jiji la Trabzon, Abdulcelil Oz amesema kwamba dereva wa baso hilo alipigwa risasi, baada ya awali kufikiri alipigwa jiwe. 
    Televisheni ya Fenerbahce imesema baso hilo lilishambuliwa kwa mtutu wa bunduki. Walinzi wa usalama walikwenda haraka kuliokoa gari hilo baada ya dereva kupigwa risasi na wakafanikiwa kulisimamisha salama. Hakuna mchezaji aliyeumia. 
    Five round marks can be seen on the windscreen of the Fenerbahce team bus after the attack
    Alama ya eneo ambalo ilipenya risasi katika kioo cha basi la Fenerbahce baada ya shambulio hilo The window nearest the driver was smashed during the attack on Saturday night
    Kioo cha karibu na dereva kilivunjika kabisa kwa shambulio hilo

    "Hali halisi ya sasa ni kwamba basi lilishambulia kwa mtutu," amesema Oz. "Ni mapema mno kusema chochote cha kufafanua, lakini kilichotokea ni risasi iliyorushwa kutoka kwa bunduki,". 
    Kiungo wa zamani wa Liverpool, Dirk Kuyt alikuwa miongoni mwa wachezaji 40 na Maofisa waliokuwapo kwenye basi hilo lililoshambuliwa karibu na mji wa Trabzon. 
    Dereva wa basi alipata maumivu kichwani na akakimbizwa hospitali. Hakuna mchwzaji aliyejeruhiwa, klabu hiyo imethibitisha.  
    Shambulio hilo lilikuja saa kadhaa baada ya Fenerbahce kushinda mabao 5-1 dhidi ya timu ya Black Sea, Caykur Rizespor katika Super Lig ya Uturuki. 

    PICHA ZAIDI NENDA: http://www.dailymail.co.uk/sport/football/article-3025939/Fenerbahce-team-coach-shot-armed-gang-way-away-game.html#ixzz3WPYy969V 

    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: BASI LA FENERBAHCE LASHAMBULIWA KWA MTUTU WA BUNDUKI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top