KOCHA Arsene Wenger amemthibitisha Mikel Arteta kuwa Nahodha mpya wa Arsenal kufuatia kumuuza Thomas Vermaelen kwa Barcelona FC.
Kocha huyo wa The Gunners, ambaye aliishuhiudia timu yake ikiwafumua mabao 3-0 mabingwa wa England, Manchester City katika mchezo wa Ngao ya Jamii jana, alilazimika kuwa na Nahodha mpya baada ya aliyekuwa Nahodha wake, Vermaelen kutimkia Barcelona.
Mustakabli wa Arteta katika klabu bado hauko wazi sana, lakini inaonekana kwa kukabidhiwa uongozi wa wachezaji wenzake, mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 32 atabaki Arsenal msimu huu. Per Mertesacker ameteuliwa kuwa Nahodha Msaidizi.



.png)
0 comments:
Post a Comment