• HABARI MPYA

    Wednesday, January 01, 2014

    MAN UNITED WATAKA KUSAJILI BONGE LA KIUNGO LA URENO

    KLABU ya Manchester United inataka kumsajili kiungo wa Sporting Lisbon ya Ureno, William Carvalho.
    United imekuwa ikisaka kiungo mkabaji sehemu mbalimbali na kwa mara nyingine, wasaka vipaji wake walishuhudia mechi ambayo Sporting ilitoka sare ya 0-0 na Porto jioni ya Jumapili, kwa mujibu wa A Bola.
    Taarifa nchini Ureno zinasema kwamba, United sasa tayari imekwishamshuhudia mchezaji huyo katika mechi saba za mzunguko wa kwanza, na kocha David Moyes anamtaka kuimrisha safu yake ya kiungo.
    Mtu wa nguvu: Carvalho amekuwa akifuatiliwa na United katika mechi kadhaa msimu huu
    In the middle: Carvalho has a release clause of around £37.5million, though United may look for a cheaper deal
    Katikati ya dimba: Carvalho ana thamani ya Pauni Milioni 37.5, ingawa United wanamtaka kwa bei poa

    Carvalho, mwenye umri wa miaka 21, aliichezea mechi ya kwanza Ureno katika hatua ya mwish ya kufuzu Kombe la Dunia mwakani, dhidi ya Sweden mwezi November na anatarajiwa kuwapo katika kikosi kitakachokwenda mjini Paulo, Brazil kwenye fainali hizo.
    Mkataba wake unamalizika mwaka 2018 na inafahamika ana thamani ya Pauni Milioni 37.5, ingawa United watatumaini kumpata kwa bei poa.
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: MAN UNITED WATAKA KUSAJILI BONGE LA KIUNGO LA URENO Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top