• HABARI MPYA

    Sunday, December 01, 2013

    ROONEY AINUSURU MAN UNITED NA KIPIGO CHA SPURS

    MABAO mawili ya Wayne Rooney leo yameinusuru Manchester United kulala mbele ya kikosi cha Andre Villas-Boas, Tottenham baada ya kupata sare ya 2-2 Uwanja wa White Hart Lane katika mchezo wa Ligi Kuu ya England.
    Kyle Walker alifunga kwa mpira wa adhabu dakika ya 18, lakini beki huyo wa kulia wa England akamsetia Rooney kuisawazishia Manchester United dakika ya 32.
    Villas-Boas alikaribia kupata ushindi baada ya Sandro kufunga bao la pili umbali wa mita 25 akimtungua kipa David De Gea dakika ya 54, lakini Rooney akasawazisha tena kwa penalti dakika ya 57.
    Kikosi cha Tottenham kilikuwa: Lloris, Walker, Dawson, Chiriches, Vertonghen, Sandro, Paulinho, Lennon/Townsend dk65, Dembele, Chadli/Sigurdsson dk84 na Soldado/Defoe dk71.
    Man United: De Gea, Smalling, Vidic, Evans, Evra, Cleverley, Jones, Valencia/Nani dk83, Kagawa/Young dk83, Welbeck/Hernandez dk72 na Rooney.
    Mkombozi: Mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney akiisawazishia timu yake kwa penalti dhidi ya Spurs
    Roo beauty: Rooney celebrates scoring United's second goal from the penalty spot against Tottenham
    Rooney akisngilia baada ya kuifungia United
    White Hart Lane roar: Sandro celebrates with the Tottenham bench after scoring against United
    Sandro akishangilia baada ya kuifungia Tottenham 
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ROONEY AINUSURU MAN UNITED NA KIPIGO CHA SPURS Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top