KLABU ya Tottenham Hotspur imedhamiria kuifunga Manchester
United kwa mara ya kwanza katika zaidi ya miaka 10 wakati timu hizo
zitakapokutana kwenye Uwanja wa White Hart Lane Jumapili, ikifahamika kwamba
wanatakiwa kujikaza baada ya kudundwa na Arsenal katika mechi iliyopita.
Katika mechi hiyo dhidi ya United inayoshika nafasi ya pili,
ikiwazidi Spurs wanaoshika nafasi ya tatu pointi nane, Tottenham watawatumia kiungo
Gareth Bale, mshambuliaji Rafael van der Vaart na beki wa pembeni Kyle Walker
ambao walikuwa majeruhi na sasa wamepona.
Man United wanazidiwa pointi mbili na vinara Manchester
City.
Kocha Harry Redknapp lazima aizindue timu yake kutoka kwenye
kipigo cha mabao 5-2 walichopewa na wapinzani wao katika jiji la London, Arsenal
kwenye Uwanja wa Emirates Jumapili iliyopita, lakini kwa bahati mbaya watamkosa
Nahodha mpya wa England, Scott Parker ambaye anatumikia adhabu.
Alipoulizwa kama Tottenham wapo kwenye nafasi nzuri ya
kuwafunga United tangu walipoifunga mara ya mwisho mwaka 2001, Redknapp alisema:
"Bado ni ngumu. Manchester United bado ni timu kubwa,”alisema.
Spurs inawazidi wapinzani wao katika jiji la London, Arsenal
na Chelsea kwa pointi saba katika vita ya kuwania nafasi ya tatu, ambayo moja
kwa moja inatopa nafasi ya kucheza Ligi ya Mabingwa na Redknapp alisema kwamba kipaumbele
kilikuwa ni kutwaa taji la Ligi kwa mara ya kwanza tangu 1961, ingawa sasa
matumaini yamepungua kutokana na matokeo yao ya karibuni.



.png)
0 comments:
Post a Comment