WAPINZANI wa Simba SC katika Kombe la Shirikisho, Kiyovu
Sport ya Rwanda wamewasili leo tayari kwa mechi ya marudiano ya Raundi ya
Kwanza dhidi ya Wekundu wa Msimbazi.
Kiyovu wanawasili wakati wenyeji wao Simba, wamekusanya
wachezaji wao wote waliokuwa timu za taifa za Uganda na Tanzania kwa ajili ya
mechi za kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika mwakani na
kuwaunganisha kambini na wenzao Bamba Beach, Kigamboni, Dar es Salaam.
Timu hizo zilizotoka sare ya 1-1 kwenye mchezo wa kwanza
Kigali, Rwanda, zinatarajiwa kurudiana Jumapili kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es
Salaam.
Wachezaji wa Simba ambao waliokuwa timu za taifa ni Juma
Kaseja, Juma Nyosso, Kelvin Yondani,
Jonas Gerald, Nassor Masoud ‘Chollo’, Shomari Kapombe, Mwinyi Kazimoto na Uhuru Suleiman waliokuwa
kwenye kikosi cha Taifa Stars kilichotoa sare ya 1-1 na Msumbiji na Emanuel
Okwi aliyekuwa kwenye kikosi cha Uganda kilichofungwa 3-1 na Kongo Brazzaville.
Mechi hiyo itaanza saa 9.30 alasiri na itachezeshwa na refa
Yabarow Hagi Wiish atakayesaidiwa na Aweis Ahmed Nur na Abdirahman Omar Abdi,
wote kutoka Somalia, wakati refa wa akiba atakuwa Waziri Sheha wa Tanzania na
Kamisaa Jean Marie V. Hicuburundi kutoka Burundi.
Watazamaji watatakiwa kulipa Shilingi 30,000 kwa kwa viti
vya VIP A, 20,000 kwa VIP B, 15,000 kwa VIP C wakati viti vya rangi ya Chungwa ni
Sh.8,000 na rangi ya bluu na kijani Shilingi 5,000.


.png)
0 comments:
Post a Comment