
MABINGWA mara sita Afrika, Al Ahly ya Misri wamedai hawahofii kucheza kwenye Uwanja wa nyasi za bandia (Uhuru mjini Dar es Salaam) katika mechi yao ya marudiano ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya wenyeji Yanga JUmamosi wiki hii. Meneja Mkuu wa Ahly, Hossam Badri alikaririwa kwenye mtandao wa klabu hiyo mwishoni mwa wiki iliyopita akisema hawana wasiwasi kucheza kwenye nyasi za bandia. “Al Ahly haitachanganywa na kucheza kwenye uwanja wa nyasi bandia kwa sababu siyo mara ya kwanza kwetu kucheza kwenye uwanja kama huo. Tulicheza na ASEC Mimosas ya Ivory Coast na Dinamuzahrary na kupata matokeo mazuri,” alisema Badri ambaye pia ni Kaimu Mkurugenzi wa Klabu hiyo. Wiki iliyopita Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), lilikubali ombi la Yanga mchezo huo kufanyika Uwanja wa Uhuru badala ya Uwanja wa Taifa kwa vile Yanga ndiyo uwanja iliouzoea. Awali TFF ilipanga mechi hiyo kufanyika Uwanja wa Taifa, lakini Yanga ilisisitiza kutaka Uwanja wa Uhuru wakiamini utawasaidia kufuta kipigo cha mabao 3-0 katika mechi ya kwanza iliyofanyika Cairo wiki mbili zilizopita. Yanga ilidai ina uzoefu zaidi kucheza Uwanja wa Uhuru ingawa watakabiliwa na upungufu wa mashabiki watakaoingia kutokana na uwanja huo kuingiza mashabiki wasiozidi 25,000 tofauti na Uwanja wa Taifa unaoingiza mashabiki 60,000. Yanga watahitaji kufunga mabao zaidi ya matatu kufuzu raundi inayofuata kwenye michuano hiyo inayoandaliwa na Shirikisho la Soka Afrika (Caf). Wakati huohuo, jopo la viongozi wa Al Ahly litatua Dar es Salaam keshokutwa kufanya maandalizi ya ujio wa timu yao. Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwenye mtandao wao viongozi hao wataongozwa na Khalid Aldrndly, lakini hawakuweka wazi siku ya kutua kwa timu hiyo. Katika hatua nyingine kocha wa Al Ahly, Manuel Jose ameonya wachezaji wake kuhakikisha wanashinda mechi yao dhidi ya Yanga. Kocha huyo anafahamu bado mchezo haujamalizika. Aliwaambia wachezaji wake mchezo huo hautakuwa rahisi. “Utakuwa mchezo mgumu kwetu kwa sababu tunacheza ugenini, tunahitaji kuweka mtazamo na kuhakikisha tunapata matokeo mazuri,” alisema.
1 comments:
Dear friend !
1.We can offer all kinds of cigarettes. We offer safe delivery and best service,low price and good quality.
2.We have excellent customer service team, which could solve online various problems about cigarettes we provide in 24 hours.
3.We have perfect Logistics system, which guarantees all the ordered cigarettes are delivered to you in good shape as fast as possible.Communicate with us.You will be very satisfied! Hope we can do long-term business in near future.
Welcome to our website for more details.
555 cigarettes
Belomorkanal Cigarettes
Benson And Hedges Cigarettes
Bond Cigarettes
Camel Cigarettes
Chesterfield Cigarettes
Dallas Cigarettes
Davidoff Cigarettes
Dunhill Cigarettes
Epique Cigarettes
ESSE Cigarettes
Gauloises Cigarettes
Karelias Cigarettes
Kent Cigarettes
Lambert and Butler Cigarettes
LM Cigarettes
Lucky Strike Cigarettes
Magna Cigarettes
Marlboro Cigarettes
Mild Seven Cigarettes
Monte Carlo Cigarettes
More Cigarettes
Muratti Cigarettes
Newport Cigarettes
Pall Mall Cigarettes
Parliament Cigarettes
Peter I Cigarettes
R1 Cigarettes
Rothmans Cigarettes
Russian Style Cigarettes
Salem Cigarettes
Sobranie Cigarettes
Sovereign Cigarettes
Special Offer Cigarettes
Viceroy Cigarettes
Virginia Slims Cigarettes
Vogue Cigarettes
West Cigarettes
Winston Cigarettes
Best regards! Thank you !
Post a Comment