• HABARI MPYA

    Saturday, March 14, 2009

    ARSHAVIN, EBOUE WAIPA USHINDI MNONO ARSENAL



    LONDON, Uingereza
    EMMANUEL Eboue wa Ivory Coast na Mrusi Andrey Arshavin (pichani) leo wameibuka mashujaa wa Arsenal baada ya kila mmoja kuifungia timu hiyo mabao mawili katika mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Blackburn wakati timu yao ikishinda 4-0.
    Arshavin alifunga bao la kwanza katika dakika ya kwanza baada ya kuitumia vizuri pasi ya Theo Walcott na kuindika bao lake la kwanza kwa Arsenal.
    Mrusi huyo aliyesajiliwa Arsenal Januari mwaka huu aliandika bao la pili dakika ya 65 safari hii akiitumia vizuri pasi ya Denilson, wakati Eboue aliyeingia kipindi cha pili alifunga bao la tatu dakika za 88 na la nne dakika ya 90 kwa kwa mkwaju wa penalti.

    MATOKEO YA MECHI ZOTE ENGLAND

    Man United Vs Liverpool 1-4
    Arsenal Blackburn 4-0
    Bolton Vs Fulham 1-3

    Everton Vs Stoke 3-1
    Hull Vs Newcastle 1-1
    M/brough Vs Portsmouth 1-1
    Sunderland Vs Wigan 1-2
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: ARSHAVIN, EBOUE WAIPA USHINDI MNONO ARSENAL Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top