• HABARI MPYA

    Thursday, December 15, 2022

    SIMBA, YANGA NA AZAM ZATENGANISHWA KOMBE LA MAPINDUZI


    MABINGWA watetezi, Simba SC wamepangwa Kundi C pamoja na Mlandege na KVZ katika michuano ya Kombe la Mapinduzi inayotarajiwa kuanza Januari 1 hadi 13, mwakani.
    Kwa upande wao, mabingwa wa Bara, Yanga SC wao wapo Kundi B pamoja na Singida Big Stars na wenyeji, KMKM ambao pia ni mabingwa wa Ligi Kuu ya Zanzibar.
    Kundi A linaundwa na Azam FC ya Dar es Salaam, wenyeji, Malindi SC na Jamhuri FC ya Pemba, wakati Kundi D kuna Namungo ya Lindi, Aigle Noir ya Burundi na Chipukizi ya Pemba.
    RATIBA KOMBE LA MAPINDUZI
    Januari 1, 2023

    Mlandege v KVS Saa 10:15
    Malindi SC v Jamhuri Saa 2:15
    Januari 2, 2023
    Namungo v Chipukizi Saa 10:15
    Singida BS v KMKM Saa 2:15
    Januari 3,2023
    Azam FC v Malindi SC Saa 10:15
    Simba SC v Mlandege Saa 2:15
    Januari 4, 2023
    Chipukizi v Aigle Noir Saa 10:15
    Yanga SC v KMKM Saa 2:15
    Januari 5, 2023
    Jamhuri v Azam FC Saa 10:15
    KVZ v Simba SC Saa 2:15
    Januari 6, 2023
    Namungo v Aigle Noir Saa 10:15
    Yanga SC v Singida BS Saa 2:15
    Januari 8, 2023
    NUSU FAINALI 1 
    Saa 2:15
    Januari 9, 2023
    NUSU FAINALI 2 
    Saa 2:15
    Januari 13,2023
    FAINALI 
    Saa 2:15
    (Nusu Fainali ya kwanza ni mshindi wa Kundi A dhidi ya mshindi Kundi B na ya pili ni mshindi wa Kundi C dhidi ya mshindi wa Kundi D).
    • Blogger Comments
    • Facebook Comments

    0 comments:

    Item Reviewed: SIMBA, YANGA NA AZAM ZATENGANISHWA KOMBE LA MAPINDUZI Rating: 5 Reviewed By: Mahmoud Bin Zubeiry
    Scroll to Top